Baada ya Denmark,Azzam, Kwale United , Kombani Youth,Mshale, Kitivo, Dumna na Kundutsi kutinga raundi ya 16 bora kwenye mechi zao za wikendi iliyopita kwenye ligi ya Rashid Abdalla Super Cup, wikendi hii kutagaragzwa mechi nyengine nane za kutamatisha hatua ya makundi kwenye ligi hiyo.

Na siku ya Jumamosi saa tisa na nusu kutapigwa mechi nne katika viwanja mbalimbali huko Kwale.

Uwanjani Waa Black Eagles watamenyana na Lazium fc.

Kwale Teachers wakabane koo na Wayzata Boys FC katika uwanja wa Kombani .

Marika FC watoane kijasho na Rsing Stars katika uga wa Mkokoni.

Katika uga wa Denmark hapo maganyakulo Lutembe watavaana na Vivah Manyota FC.

Siku ya Jumapili itakua zamu ya Albion Youth kumenyana na Desert FC kwenye uwanja wa Mkokoni.

Fafada Fc watakua katika uchanjaa wa Waa kubwagana na Bongwe United.

Wailers FC watakipiga dhidi ya FC Talibase uwanjani Denmark Maganyakulo.

Katika uga wa Kombani Morocco watamenyana na Green Boys FC .

Mechi zote za jumapili zitaanz asa atisa na nusu.