Baraza la CIPK kukabiliana na utumizi wa mihadarati
Baraza la maimamu na wahubiri nchini Kenya CIPK limesema litashirikiana na washika dau mbali mbali ili kukabiliana na donda sugu la utumizi wa mihadarati.
Akizungumza na wanahabari hapa Mombasa katika ofisi za baraza hilo, katibu mkuu wa baraza hilo sheikh Mohammed Khalifa amesema kuwa vita dhidi ya mihadarati vinahitaji juhudi za pamoja.
Khalifa ametaka asasi za kiserikali kuendeleza vita dhidi ya mihadarati hadi katika dawa zengine za kulevya.
Aidha Khalifa amesema kwamba utumiaji wa dawa za kulevya umekua janga sugu nchini Kenya, huku akisema kuwa fedha nyingi zinatumika kila siku katika biashara hio.
Kwa upande wake sheikh Mohammed Dori ameshangazwa na hatua ya kupigwa marufuku kwa bhangi na kuhalalishwa kwa miraa huku akisema athari zote ni sawa.