Inspekta Jenerali wa Polisi, Japhet Koome ametaja maandamano ya madaktari na maafisa wa kliniki kama usumbufu kwa umma.

Kulingana na Koome, watabibu hao wamekuwa wakilala barabarani na hivyo kuzuia barabara kuu, barabara za umma na kutatiza mtiririko wa magari na harakati za watu wakati wa maandamano yao.

Koome amesema kuwa matabibu hao wameshiriki maandamano hayo bila kuwafahamisha maafisa wa polisi, jambo ambalo ni kinyume na sheria za Kenya.
Aidha amesema kuwa wasio madaktari, ambao wana nia ya kusababisha maafa kwa umma wanakusudia kujiunga na maandamano yanayoendelea.

Sasa madaktari wametakiwa kufanya maandamano hayo kwa tahadhari, kwani kitendo chochote cha kuvunja haki za umma hakitavumiliwa.

Kwa hiyo kwa maslahi ya usalama wa taifa, Makamanda wote wa Polisi wameagizwa kushughulikia hali hizo kwa uthabiti na kwa mujibu wa sheria. Tunataka kuwaonya madaktari wote kujiepusha na kukiuka haki za wengine wanapoandamana, na kwamba juhudi zao za kutatiza utendakazi mzuri wa hospitali hazitavumiliwa,” Koome akasema.

Ni mwezi mmoja tangu madaktari waanze mgomo, na wamekuwa wakiandamana kudai kuajiriwa kwa madaktari wanajenzi na utekelezaji wa makubaliano mengine katika CBA ya mwaka 2017.

Kwa upande mwingine, maafisa wa kliniki wako katika wiki yao ya pili ya mgomo, wakitoa matakwa sawa.
Wakiongozwa na miungano yao, Chama cha Madaktari, Wanafamasia, na Madaktari wa Meno (KMPDU) na Muungano wa Maafisa wa Kliniki nchini (KUCO), madaktari hao wameapa kutolegeza Kamba hadi serikali itimize matakwa yao.

Juhudi za serikali, kupitia Wizara ya Afya na Mkuu wa Utumishi wa Umma Felix Koskei, kujadili mbinu ya kurejea kazini kwa madaktari hazijafaulu.

Ni mwezi mmoja tangu madaktari washushe zana zao, na wamekuwa wakiingia barabarani kudai kutumwa kwa wafanyikazi na utekelezaji wa makubaliano mengine katika CBA ya 2017.

Kwa upande mwingine, maafisa wa kliniki wako katika wiki yao ya pili ya mgomo, wakitoa matakwa sawa.

Wakiongozwa na miungano yao, Chama cha Madaktari, Wafamasia, na Madaktari wa Meno (KMPDU) na Muungano wa Maafisa wa Kitabibu wa Kenya (KUCO), madaktari hao wameapa kutolegea hadi serikali itimize matakwa yao.

Juhudi za serikali, kupitia Wizara ya Afya na Mkuu wa Utumishi wa Umma Felix Koskei, kujadili fomula ya kurejea kazini na madaktari hazijafaulu.


 

More Stories

Buriani jenerali Francis Ogolla

Idara ya polisi yasema mgomo wa madaktari ni usumbufu

Seneta Miraj amtetea waziri wa afya

Bandari ya Lamu kuipiku ile ya Mombasa asema Mbogo