Chama cha ODM kimependekeza kuondolewa kwa mbunge wa Rarieda Otiende Amollo kutoka Kamati ya Haki na Sheria ya Bunge.

Mbunge wa Ruaraka TJ Kajwang atachukua nafasi ya Otiende katika JLAC inayoongozwa na Mbunge wa Kangema Muturi Kigano.

Otiende kwa sasa ni Naibu Mwenyekiti wa JLAC iliyojadili juu ya Muswada marekebisho ya Katiba ya Kenya (Marekebisho), 2020.

Lakini mbunge huyo wa Rarieda baadaye kwenye Twitter na kulaumu matapeli wa kisiasa kwa kuwa nyuma ya hoja hiyo ya kubanduliwa kwake.

Bunge la kitaifa Alasiri liliidhinisha hoja ya kutaka kuundwa upya kwa kamati zingine pamoja na JLAC ambapo Amollo alibadilishwa.