Nyota ya Mlinda lango Chuma Mohammed inaendelea kung’aa baada ya kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa Harambee stars chini ya umri wa miaka 20.

Mwaka 2023 umekua mzuri kwa Chuma baada ya kutwaa tuzo ya kipa bora pamoja na kusaidia timu yake ya Mombasa Maize Millers kuwa mabingwa wa Taifa Ngano Super cup mnamo oktoba 29 katika uwanja wa Mombasa sports club .

Kipa huyo mahiri pia alitamba katika michuano inayoendelea ya Rashid Abdallah super cup Makala ya nne akiichezea Kundutsi FC iliyobanduliwa na Wailers katika hatua ya robo fainali.

Chuma ameiwakilisha kaunti yay a Mombasa kwenye michuano ya talanta hela kwa wachezaji wasizidi umri wa miaka 19.

Kwenye michuano hiyo ya Talanta hela kanuti ya Mombasa ilitolewa na kaunti ya homa baya kwenye hatua ya robo fainali.

Homa bay ndio mabingwa wa talanta hela baada ya kuichapa Kisumu mabao 4-2 kwenye fainali iliyopigwa katika maadhimisho ya 60 tangu kupata uhuru siku ya jumanne katika uwanja wa nyayo.

Kwenye michuano hiyo ya Talanta hala Chuma aliandikisha cleansheet nyingi kuliko kipa kipa yeyote .

Rahma Viwanjani inamtakia kila la heri kipa Chuma Mohamed.


 

More Stories

Miraa na Mgoka kupigwa marufuku Mombasa

Wanafunzi kurudi shuleni juma lijalo

Vita dhidi ya mihadarati vyapamba moto Pwani