Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la soka nchini Cameroon, imetupilia mbali barua ya kujiuzulu ya Rais wa Shirikisho hilo Samuel Eto’o.

Ombi la Samuel Eto’o kujiuzulu kama Rais wa FECAFOOT limekataliwa na kamati Utendaji bila kujali mwenendo mbaya wa timu ya Taifa ya Cameroon nchini Ivory Coast kwenye michuano ya AFCON.

Kamati hiyo bado inaamini kuwa Eto’o anasalia kuwa mtu sahihi kuongoza Shirikisho hilo.

Samuel Eto’o anashutumiwa katika upangaji wa matokeo na vitisho kwa wachezaji wa timu ya taifa ya Cameroon.