Nigeria kuminyana na Ivory Coast katika fainali ya AFCON huku Afrika kusini wakisaka nafasi ya tatu dhidi ya Jamhuri ya kidemokrasia Congo.

Mtanange wa kumtafuta mshindi wa tatu wa AFCON kati ya Afrika Kusini na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo itapigwa jumamosi saa tano usiku huku fainali ikigaragzwa jumapili kati ya wenyeji Ivory Coast na Nigeria.

Wenyeji Ivory coast mara ya mwisho kushinda kombe la AFCON ilikua mwaka 2015 wakiongozwa na nahodha Yaya Toure huku wapinzani wao Nigeria walishinda taji hilo la AFCON 2013.

Nigeria walitingia fainali baada ya kushinda mechi yao ya nusu fainali dhidi ya Afrika kusini kupitia mikwaju ya penalti, nao Ivory coast waliipiga Congo goli moja bila jawabu lililofungwa na mchezaji Sebastian Haller.


 

More Stories

Buriani jenerali Francis Ogolla

Idara ya polisi yasema mgomo wa madaktari ni usumbufu

Seneta Miraj amtetea waziri wa afya

Bandari ya Lamu kuipiku ile ya Mombasa asema Mbogo