Serikali ya kaunti ya Mombasa imetakiwa kutenga sehemu maalum kuwa soko la watu wenye ulemavu kuweza kuuza bidhaa zao.

Kulingana na mkurugenzi mkuu wa shirika la watu wenye ulemavu la Tunaweza Women with Disability,Charity Chahasi, walemavu kaunti ya Mombasa ni wengi ila hawana sehemu ya kufanya biashara hivyo wengi ujikuta barabarani wakiomba.

Ametaja kutengwa kwa sehemu hio kuwa itasaidia watu wenye uemavu kufanya biashara na kujikimu kimaisha.