Kongamano la kujadili uchumi wa baharini lakamilika huku hamasisho zaidi zikitolewa kupiga jeki juhudi hizo

Kongamano la kujadili mbinu za kuboresha uchumi wa baharini baina ya mataifa wanachama wa IGAD limekamilika rasmi hapa jijini Mombasa.Kongamano hilo la siku nne liliwaleta pamoja wawakilishi kutoka...

Hatimaye muungano wa mabaharia nchini SUK waandaa uchaguzi wake

Hatimae Muungano wa mabaharia nchini SUK umeandaa uchaguzi wake rasmi katika ukumbi wa Licodep eneo bunge la Likoni kama ilivyoratibiwa baada ya uamuzi wa mahakama ya leba.Katika uchaguzi huo,...

Mashirika ya kijamii hapa Mombasa yamewasilisha amri ya mahakama kwa ofisi ya gavana wa Mombasa na kwa bunge la kaunti kushinikiza kuundwa kwa sheria itakayofanikisha makongamano ya bajeti.

Wakizungumza na wanahabari baada ya kuziwasilisha nakala hizo, mwenyekiti wa mashirika ya kijamii hapa Mombasa Zedekiah Adika amesema tangu serikali za ugatuzi, bunge la kaunti ya Mombasa limekuwa likipasisha bajeti na sheria mbalimbali bila kufuata taratibu zinazostahiki ikiwemo kuhusisha vikao vya umma.

Kulingana nao pesa zimekuwa zikitumika kinyume na sheria kutokana na ukosefu wa sheria hiyo na walienda mahakamani kushinikiza taratibu hizo kufutwa.

 Aidha wanataka taratibu za bajeti ya mwaka wa kifedha 2022/2023 kutoandaliwa iwapo sheria hiyo haijatengengenezwa.

Kitengo hicho kinahusisha wananchi wanaoteuliwa kisheria pamoja na mawaziri wa kaunti.

Mashirika hayo yamesema kuwa iwapo halitatekelezwa watalazimika kurudi mahakamani ili kuona kuwa wahusika wanachukuliwa hatua za kisheria.

Mwandishi: Ibrahim Juma


RadioRahma ads