Skyward Express yafadhili mashindano ya mbio za half marathon Kwale
Klabu ya Kick Martial Arts kutoka Ukunda ikishirikiana na shirika la ndege la skyward express wataandaa mashindano ya mbio za half marathon iliyopewa jina la “the Kick out Unfitness” itakayoanza kesho jumamosi .
Lengo la mbio hizo ni kusaidia na kuhakikisha kuwa vijana wamekuzwa katika nyanja ya michezo,kuboresha afya zao na kujishughulisha na masuala muhimu katika jamii.
Kulingana na shirika hilo la ndege la Skyward linaamini kwamba vijana ndio viongozi wa siku za usoni,hivyo basi kuna haja ya kukuza na kusaidia vipaji vyao kwa kila njia
Zaidi shirika hilo limesema kwamba ni kutokana na kuongezeka kwa wateja wao huko Diani tangu waanzishe safari zao mwaka wa 2018 na ushirikiano mwema na wakazi wa kaunti ya Kwale ndio maana wanaandaa michezo kama hiyo ili kuregesha shukrani kwa wakazi hao.
Huku wakiwa na matumaini kuwa mashindano hayo ya mbio yataafikia malengo yake na kukua zaidi katika siku zijazo.