Uwanja wa Royal Golf Club kaunti ya Nairobi utakua mwenyeji wa mashindano ya Safaricom Golf Tour mkondo wa 14.

Michuano hiyo ya wikendi ambayo ni ya mwisho kabla ya fainali zitakazopigwa wiki ijayo huko Vipingo Ridge, imevutia zaidi ya washiriki 350 .

Michuano hiyo ya kishirika imeratibiwa kufanyika jumamosi huku ile ya chipukizi ikifanyika jumapili.

Kulingana na mkurugenzi mkuu Peter Ndegwa anafurahia hatua walizopiga za kutambua wachezaji wadogo wenye talanta miongoni mwa chipukizi.

Ndegwa ameeleza kuwa wamehusisha zaidi ya washiriki 8, 000 kupitia michuano hiyo, hamasa, na mafunzo ya mchezo huo wa golf uyaliyojumuisha chipukizi 5, 000.

Wikendi iliyopita Nelson Nyoike aliwagaragaza wachezaji golf 253 na kushinda taji la awamu ya 13 uwanjani Vet Lab Golf Club.

Belinda Wanjiru wa miaka 12 na Beiju Shah wa miaka 16 walitawazwa washindi kwenye michuano ya chipukizi baada ya kuwabwaga wachezaji 165 katika uchanjaa huo wa Vet Lab Golf Club .

Michuano hiyo ya wikendi itajumuisha mashindano ya kishirika siku ya jumamosi pamoja na mpango wa uhamasisho unaofahamika kama “Golf Mataani”, ambapo wachezaji wachanga kutoka jamii jirani watapata nafasi ya kujifunza kuhusu mchezo huo wa golf.

Safaricom imewekeza shilingi milioni 100 katika Makala ya uzinduzi wa ziara hiyo kwa lengo la kukuza talanta ya gofu.

Safaricom Golf Tour imefanyika katika viwanja 13 vya golf humu nchini ikiwemo viwanja vya Nanyuki, Limuru, Muthaiga, Nyanza, Machakos, Eldoret, Keren, Nyali, Kericho, Kitale, Nakuru, Kenya Airforce na Vetlab.

Ziara hiyo ya mchezo wa golf itatamatika Vipingo Ridge kaunti ya Kilifi ambako kutapigwa fainali ambapo washindi kutoka kila awamu watapigania tuzo kuu.

Klabu ya Bandari FC imekamilisha usajili wa wachezaji wawili Omar Somobwana na Mohammed Abeid Mudiga.
Somobwana na Abeid, wamejiunga na Bandari wakitokea AFC Leopards na Coastal Heroes mtawalia, baada ya kuchezea Bandari kwa mkopo.

Wawili hao wamesaini mkataba wa miaka miwili kila mmoja na wanatarajia kuboresha juhudi za Bandari kunyakua kombe la ligi kuu hapa nchini.

Katika taarifa kwa vyombo vya habari mwenyekiti wa kamati ya kiufundi wa Bandari Musa Hassan amesema kuwa wawili hao ni kielelezo cha falsafa ambayo itahakikisha maisha marefu ya Bandari.

Somobwana ni beki mahiri kutoka kaunti ya Lamu na amechezea timu za taifa ya vijana chini ya miaka 17 na 20, akiwa katika shule ya upili ya wavulana ya St Anthony kaunti ya Kitale.

Kwa upande wake Omar alisajiliwa na AFC Leopards mwaka 2020 na amekuwa mmoja wa chipukizi wakuu katika timu ya vijana chini ya kocha Patrick Aussems.

Hassan amesema wachezaji hao wawili ni sajili za kwanza miongoni mwa wachezaji wanaotarajiwa kusajiliwa na Bandari.

Wakati uo huo klabu hiyo ya Bandari imethibitisha kuondoka kwa viungo Collins Agade, ambaye ni mchezaji huru na Danson Namasaka aliyejiunga na KCB.

Bandari pia imewaita wachezaji wake Wilberforce Lugogo na Hamid Mohammed baada ya kuchezea Sofapaka kwa mkopo wa mwaka mmoja.

Wawili hao watajiunga na timu ya Bandari kwenye matayarisho yao ya msimu ujao.

 

Tuanze na ratiba ya mechi kadhaa za ligi ya fkf kaunti ya kwale zitakazopigwa wikendi 23/07/2022

Jumamosi 23/07/2022 Rafiki Boys FC watakuwa mwenyeji wa Kwale United katika uwanja wa Makongeni saa tisa alasiri.

Vanga United watakaokuwa kwenye uchanjaa wao wa nyumbani wa Kiwegu watapepetana na Denmark saa tisa alasiri.

Jumapili 24/07/2022 kutagaragzwa mechi tatu Diani Stars watavaana na Nuru United FC mapema saa tano katika uga wa Jogoo.

FC Vienna wataikaribisha Schlke04 Fc uwanjani Kiweke saa tisa alasiri.

Saa tisa alasiri kwenye uga wa Kombani kutashuhudiwa ngarambe baina ya wenyeji Kombani Youth FC na wageni wao Orlando Pirates FC.

Na kwenye mechi za ligi ya daraja la pili kaunti ya Mombasa

Alidina youth watamenyana na Shatters uwanjani Bomu saa nane mchana.

Young heroes watoane kijasho na Leeds utd saa nane katika uwanja wa Mwahima .

Saa kumi alasiri Freedom fighters watabwagana na mgeni wao Shikaadabu katika uga wa Peleleza .

Siku ya jumapili Msa phoenix watakabiliana na Eleven stars katika uga wa Tononoka sa nane mchana sawa na Mkunguni

watakaobwagana na Kitaka youth katika uwanja wa Mbuzi .

Changamwe wazee watashuka dimbani saa kumi alasiri kupepetana na Hippo rangers .

Wayani utd watakuwa mbele ya mashabiki wao wa nyumbani uwanjani Wayani saa kumi alasiri kukabiliana na Wazee health

Show more post