Waziri wa utalii na biashara kaunti ya Kwale Michael Mutua amewataka wafanyibiashara wa Ukunda wanaohudumu kando kando mwa barabara kuhamia katika soko jipya lililojengwa na serikali ya kaunti hiyo.

Akizungumza katika ziara ya ukaguzi wa soko hilo, Mutua ameagiza kusikitishwa kwa shughuli zote za kibiashara zinazoendelezwa kando ya barabara kuu ya Likoni - Lungalunga kwa usalama wa wafanyibiashara hao.

Kauli ya waziri huyo inajiri baada ya baadhi ya wafanyibiashara wa soko la Ibiza na Kalipso kudinda kuhamia katika soko jipya la kaunti lililoko eneo la Mvindeni.

Kwa upande wao baadhi ya wafanyibiashara waliohamia katika soko hilo wamewarai wenzao kujiunga nao ili kuendeleza shughuli zao pamoja.

Wakiongozwa na Juma Malombe, wafanyibiashara hao wameelezea kuridhishwa kwao na jinsi hali ya usalama imeimarishwa katika soko hilo.

Kampuni ya kusaga unga wa mahindi na ngano ya Kitui Flour Mills inayomiliki chapa ya Unga wa Dola imezindua bidhaa yao mpya sokoni ya mafuta ya kupikia.
Mafuta hayo ya kupikia ya Dola yanakuwa bidhaa ya hivi karibuni kuingia katika chapa za kampuni hiyo kama moja wapo ya mikakati yake ya kufikia mahitaji ya wateja ya kupata chakula chenye ubora wa hali ya juu.
Uzinduzi wa mafuta hayo ya kupikia katika kiwanda chake eneo la Vipingo kaunti ya Kilifi umesaidia uboreshaji wa uchumi katika eneo hilo kupitia uzalishaji wa ajira.
Mkurugenzi wa fedha wa kampuni hiyo Anwar Bajaber amedokeza kuwa uzinduzi wa bidhaa hiyo unaoenyesha kujitolea kwao katika soko la humu nchini kwa Zaidi ya miaka 50.
Bajaber ameeleza kuwa wataendelea kuwekeza humu nchini wakitoa kipau mbele katika sekta ya chakula na kwamba wako makini kufanya kazi na washirika pamoja na wawekezaji.
Soko la mafuta ya kupikia linatarajiwa kuongezeka kimapato kwa asilimia 13.37 pamoja na asilimia 4.75 kwa uzalishaji wake katika kipindi cha mwaka 2023 hadi 2028, hii ikiwa ni kulingana na takwimu za utafiti na soko.
Haya yanajiri huku ununuzi wa mafuta ya kupikia ukiendelea kuongezeka kutokana na ongezeko la idadi ya watu, ongezeko la miji na shughuli za kiuchumi baada ya janga la korona.

 

Mwezi wa Ramadhan umekua msimu wa biashara kwa wanabiashara wanaouza nazi katika maeneo mbali mbali hapa Pwani.

Bidhaa hiyo ambayo imekua hadimu sasa imekua ikiuzwa kati ya shilingi 70 hadi 150.
Kulingana na Hamza Mohammed ambae ni mkulima wa nazi kauti ya Kwale ameeleza kuwa bidhaa hiyo imekua hadimu kutokana na kiangazi kirefu kilichoshuhudiwa mwaka uliopita sambamba na kuimarika kwa soko la bidhaa hiyo humu nchini na hata nchi Jirani ya Tanzania.
Ameeleza kuwa bado biashara hiyo inaendelea kushamiri ingawa inapatikana kwa ugumu mashambani
Hata hivyo kwa wanaouza bidhaa za vyakula wameeleza kughadhabishwa na kupanda kwa bidhaa ya nazi wakisema kuwa inatia hasara huku wengine wakishindwa kuendeleza bishara hizo.
Waliotajwa kuathirika zaidi ni wafanyibishara wa mikate ya sinia wakisema kuwa nazi ni kiungo muhimu kwa biashara hiyo lakini kupanda kwake kumechangia faida ndogo katika biashara hiyo.

Kampuni ya HF Group imetangaza faida ya shilingi milioni 256.7 baada ya kuandikisha hasara ya shilingi milioni 682.7 mwezi Disemba mwaka 2021.

Faida hii inaashiria ukuwaji wa asilimia 939 baada ya kuboreshwa kwa mikakati ya kibiashara.

Kulingana na afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo Robert Kibaara ukuwaji huu umetokana na utendakazi wa huduma za benki za kampuni hiyo ambapo faida yake ilikua kwa asilimia 560 baada ya ushuru hadi shilingi milioni 178.2 kutoka kwa hasara ya shilingi milioni 381.3 mwezi Disemba mwaka 2021.

Vile vile mapato ya riba yaliongezeka kwa shilingi bilioni 3.6 huku ukuwaji wa mali ukiongezeka kwa asilimia 10 kutoka kwa asilimia 9.6 mwezi Disemba 2021.

Mapato ya riba yaliongezeka kwa shilingi milioni 347 huku malipo ya riba yakikuwa kwa asilimia moja ambayo ni sawa na shilingi milioni 15.

Kibaara ameeleza matumaini ya shirika hilo kuendelea kuandikisha faida katika vitengo vyake vyote vya biashara.

Ameeleza kuwa mwaka huu wa 2023, wanalenga kuimarisha huduma za zao za kifedha hususan kwa wafanyibiashara wadogo kwa kuwapa fedha kuendeleza biashara.

 

Show more post