Msimamizi wa timu ya Kadzandani inayoshriki ligi ya primia hapa Mombasa, Lucy Abuna anahofia kwamba huenda timu yake isishiriki kwenye mechi zao zilizosalia katika ligi hiyo ya primia kutokana na changamoto za kifedha.

Akiongea na Radio Rahma Abuna amesema wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kushindwa kulipa pesa ya refa kwa kukosa mdhamini.

Ameongeza kuwa imekua vigumu kwake kumudu timu hiyo licha ya wachezaji wake kujitahidi kushinda ligi ya daraja la kwanza na ligi ya daraja la pili kabla ya kupanda daraja na kutinga ligi ya primia ambayo wanacheza kwa sasa.

Kwa sasa anawaza kuhusu kuachana na soka na huenda pia timu yake ikatoka kwenye ligi hiyo ya Mombasa .

Lucy ameongeza mara nyengine wachezaji wake hulazimika kucheza bila kula na ata kutembea mguu ili kushiriki mechi za ugenini.

Ameeleza kuwa presha hupanda hususan inapofika siku ya mechi huku akiongeza kwamba licha ya juhudi za kufikia jamii na viongozi ili kupata usaidizi hazikufua dafu, ameendelea kutoa wito kwa jamii na viongozi kusaidia timu hiyo.Kwenye mechi yao ya wikendi Kadzandani waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya wenyeji wao Wanderers na wikendi hii ya tarehe 27 Mei wameratibiwa kupepetana na Daytona saa tisa unusu .

Kadzandani inavuta mkia kwenye msimamo wa ligi ya primia Mombasa ikiwa na alama tatu baada ya kupiga mechi saba.

Ligi hiyo ya Mombasa ina timu 16.

 

Mvita young stars wanaongoza ligi ya primia hapa Mombasa ikiwa na alama 15 baada ya kucheza mechi 5 ikifuatiwa na coast stars yenye alama 12 baada ya kucheza mech 5.

Cosmos inakalia nafasi ya 3 wakiwa na alama 10 sawa na Magongo Rangers pamoja na Annex baada ya kupiga mechi zake tano.

Mabingwa watetezi Goodhope wamejizolea alama 9 baada ya kucheza mechi 5.

Kadzandani inavuta mkia kwenye jedwali hilo la timu 18 wakiwa wamepoteza mechi zake zote 5 za ligi hiyo.

Likoni Combine ina alama 2 baada ya kucheza mechi 5 sawa na Mantubila.

Ligi hiyo ya primia iko chini ya chama cha soka kaunti ya Mombasa .

Baada ya Tusker kuibuka na ushindi wa bao moja dhidi ya KCB kwenye mechi yao ya ligi kuu nchini KPL katika uwanja wa Ruaraka jumatano wiki hii, Tusker na KCB zinatarajiwa kukutana tena katika ngarambe nyengine wikendi hii.

Tusker na KCB zitamenyana kwenye robofainali ya kombe la FKF kesho jumamosi,  huku mshindi wa kombe hilo akitarajiwa kupeperusha bendera ya taifa msimu ujao kwenye kombe la CAF .

Kocha wa Tusker Robert Matano ameahidi kuwa timu yake itaonyesha mchezo wa kuvutia huku akiwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kushuhudia ngarambe safi kutoka kwa wanataska .

Aidha ameeleza kuwa katika hatua hiyo ya muondoano timu yoyote inaweza kuibuka na ushindi na kuongeza kuwa kinachotakiwa ni kutumiavizuri nafasi unazopata ili kupata ushindi.

Kwa upande wake kocha wa KCB Zedekiah Otieno, amewataka wachezaji wake kuwajibika Zaidi kwenye mechi hiyo kubwa ya wikendi dhidi ya mahasimu wao Tusker.

Kwenye mechi nyengine yar obo fainali itakayopigwa jumamosi Sofapaka watakabana koo na Ulinzi stars katika uwanja uo huo wa Ruaraka baada ya ngarambe ya Tusker na KCB.

Siku ya jumapili  mechi nyengine mbili za robo fainali zitagaragazwa uwanjani Moi huko Kasarani amabpo Kakamega Homeboyz watamenyana na  Kariobangi mapema kabla ya AFC Leopards kutoana kijasho na Bandari.

Aidha haijajulikana iwapo mashabiki wa Leopards watahudhuria kwenye mtanange huo baada ya kutishia kususia ngarambe hiyo, wakipinga uamuzi wa FKF kuwapiga marufuku kuhudhuria mechi nne za ligi mapema wiki hii.

Uamuzi huo wa FKF unajiri baada mtafaruku kuzuka katika uwanja wa Bukhungu, Kakamega ambapo mashabiki wa Ingwe waliokuwa na hasira walivamia uwanja na kuibua hofu kwa mwamuzi wa kati, waliyedai kuwa ana upendeleo.

 

Katika mechi ya pili ya hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya, Inter Milan wameichapa Ac Milan mabao mawili kwa sifuri.

Kwa hatua hiyo sasa Inter wamejiweka katika nafasi nzuri katika mechi ya duru ya pili ya Jumanne ijayo.

Edin Dzeko na Henrikh Mkhitaryan walihakikishia Inter ushindi huo wa mabao mawili kwenye mechi hiyo ya jana.

Mshindi wa mechi hiyo ya jumanne ijayo atamenyana na mabingwa Real Madrid au Manchester City katika fainali itakayochezwa Instanbul Juni 10.

Picha kwa hisani

Huko Afrika Mashariki, Klabu ya Yanga kutoka Tanzania imeibuka na usindi wa mabao 2-0 dhidi ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho la soka Afrika (CAF) na kutanguliza mguu mmoja katika fainali ya michuano hiyo.

Mabao ya Yanga yalipachikwa na kiungo Stephane Aziz Ki, dakika ya 64 na Winga wao Benard Morrison dakika ya 90 na sekunde kadhaa.

Kutokana na matokeo hayo yanga inahitaji ushindi au sare katika mechi ya marudino itakayochezwa Afrika Kusini Mei 17 mwaka huu ili kutinga fainali.

Hii ni mara ya kwanza kwa Yanga kufika nusu fainali ya michuano ya CAF.

 

Real Madrid walimilika mtanange wao wa robo fainali ya ligi bingwa ulaya baada ya kuitandika Chelsea mabao 2-0 huku Ben Chilwell akionyeshwa kadi nyekundi na kulazimisha the blues kumaliza mechi hiyo wakiwa wachezaji 10 uwanjani.

Bao la kipindi cha kwanza lililofungwa na mshambuliaji nyota Karim Benzema liliwaweka Real kifua mbele na kuwamiliki Chelsea wanaongozwa na kocha Frank Lampard na mambo yalizidi kuwa magumu baada ya Chilwell kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kumchezea ngware Rodrygo nje ya kijisanduku.

Marco Asensio aliongezea Real Madrid bao la pili kwenye ngarambe hiyo.

Mmiliki wa Chelsea Todd Boehly alisikitishwa na matokeo ya mtanange huo , ambaye alikuwa Madrid akitazama mchezo huo na alitabiri kwa ujasiri ushindi wa 3-0 kwa timu yake wakati akihojiwa na ripota wa Sky Sports News Gary Cotterill kabla ya mechi.

Chelsea watavaana tena na Real Madrid jumanne ijayo kwenye mechi ya marudiano .

Show more post