Hatimaye muungano wa mabaharia nchini SUK waandaa uchaguzi wake

Hatimae Muungano wa mabaharia nchini SUK umeandaa uchaguzi wake rasmi katika ukumbi wa Licodep eneo bunge la Likoni kama ilivyoratibiwa baada ya uamuzi wa mahakama ya leba.Katika uchaguzi huo,...

Serikali ya kitaifa na kaunti zatakiwa kushirikiana kuwawezesha wavuvi kwa vifaa vya kisasa

Ipo haja ya serikali ya kitaifa na zile za kaunti kushirikiana kuhakikisha inawekeza zaidi kwa kuwawezesha wavuvi kupata vifaa kuvua katika bahari kuu.Gavana wa Lamu Issa Timamy ambaye pia ni...

Miraa na Mgoka kupigwa marufuku Mombasa

Wanafunzi kurudi shuleni juma lijalo

Vita dhidi ya mihadarati vyapamba moto Pwani

Mbunge wa Kinango Gonzi Rai amezindua ujenzi wa madarasa mawili katika shule ya Msingi ya Bumburi eneo hilo la Kinango kaunti ya Kwale.

Kulingana na mbunge huyo ujenzi huo wa madarasa mawili utagharimu takriban shilingi milioni 2.8 na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.

Gonzi amesema kuwa ujenzi wa madarasa hayo utafaidi zaidi ya wanafunzi 90 akiongeza kuwa mradi huo ni miongoni mwa mikakati yake ya kumaliza tatizo la uhaba wa madarasa katika shule hiyo pamoja na kuimarisha viwango vya elimu katika eneo hilo la Kinango.

Mradi sawia na huyo unaendelea katika shule ya msingi ya Kajiweni central wadi ya Mackinon.


RadioRahma ads