Kongamano la kujadili uchumi wa baharini lakamilika huku hamasisho zaidi zikitolewa kupiga jeki juhudi hizo

Kongamano la kujadili mbinu za kuboresha uchumi wa baharini baina ya mataifa wanachama wa IGAD limekamilika rasmi hapa jijini Mombasa.Kongamano hilo la siku nne liliwaleta pamoja wawakilishi kutoka...

Hatimaye muungano wa mabaharia nchini SUK waandaa uchaguzi wake

Hatimae Muungano wa mabaharia nchini SUK umeandaa uchaguzi wake rasmi katika ukumbi wa Licodep eneo bunge la Likoni kama ilivyoratibiwa baada ya uamuzi wa mahakama ya leba.Katika uchaguzi huo,...

Miraa na Mgoka kupigwa marufuku Mombasa

Wanafunzi kurudi shuleni juma lijalo

Vita dhidi ya mihadarati vyapamba moto Pwani

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa chanjo dhidi ya virusi vya corona iliyotengenezwa na kampuni ya Moderna inaweza kutumika kwa dharura, na kuwa chanjo ya tano miongoni mwa zilizoidhinishwa na shirika hilo ili kutumika na mataifa ulimwenguni.

WHO imesema lengo la hatua hiyo ni kuwezesha upatikanaji wa haraka wa dawa, chanjo na vifaa vya uchunguzi kukabiliana na dharura iliyopo.

Naibu Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Mariangela Simao, alisema kwamba sasa ni muhimu kuwa aina nyingi za chanjo baada ya kujitokeza kwa changamoto ya usambazaji wake ikiwemo kutoka India, taifa ambalo linakabiliwa na wimbi kubwa la maambukizo ya Covid- 19.

 Mbali ya chanjo ya Moderna, WHO pia tayari ilitoa ithibati kwa chanjo za Pfizer, AstraZeneca, Johnson & Johnson na nyingine iliyotengenezwa na taasisi moja ya India.

Kwa  Hissani ya DW SWAHILI

RadioRahma ads