Gavana wa Kwale Fatuma Achani amesema kuwa uzinduzi wa mradi wa kisima cha maji katika eneo la Melikubwa huko Macknon unalenga kukabiliana na baa la njaa katika eneo hilo ambalo hukumbwa na kiangazi kikali mara kwa mara.

Kulingana na Achani mradi huo utawasaidia wakaazi kupata maji ya mifugo na kuyatumia katika maswala ya kilimo badala ya kutegemea chakula cha msaada kutoka kwa serikali na wahisani.

Mwanaharusi Rashid na taarifa zaidi