Mwili wa afisa wa polisi wapatikana na majeraha kichwani Kibarani

Mwili wa afisa wa Polisi umepatikana umetupwa katika eneo la Kibarani hapa Mombasa. Akithibthisha kisa hicho kamanda wa polisi eneo bunge la Jomvu Lydia Wanjiru amesikitishwa na mauaji ya afisa wa...

Kongamano la kujadili uchumi wa baharini lakamilika huku hamasisho zaidi zikitolewa kupiga jeki juhudi hizo

Kongamano la kujadili mbinu za kuboresha uchumi wa baharini baina ya mataifa wanachama wa IGAD limekamilika rasmi hapa jijini Mombasa.Kongamano hilo la siku nne liliwaleta pamoja wawakilishi kutoka...

Gavana wa Kaunti ya Kwale Fatuma Achani amesema serikali yake itaendelea kuboresha Sekta ya kilimo hasa katika maeneo kame.
Achani amesema atafanikisha hilo kupitia uchimbaji wa Mabwawa ili kukabiliana na janga la njaa linalosababishwa na kiangazi katika maeneo hayo.

Kiongozi huyo amesema uchimbaji wa mabwawa 17 katika kaunti hio ikiwemo mabwawa ya Nyalani, Kizingo na Mwaluvuno huko Kinango, kumesaidia kukuza kilimo cha unyunyiziaji katika maeneo hayo, huku ekari zaidi ya 200 zikinufaika na mpango huo wa kilimo.

Kulingana na wakulima wa Kaunti hio wakiongozwa na Ndoro Nyondo, wamesema mpango huo wa uchimbaji mabwawa umewasaidia kuzalisha mazao ya kutosha.

Nyondo amesemahapo awali walilazimika kutegemea chakula cha misaada wakati wa kiangazi.


RadioRahma ads