Mwili wa afisa wa polisi wapatikana na majeraha kichwani Kibarani

Mwili wa afisa wa Polisi umepatikana umetupwa katika eneo la Kibarani hapa Mombasa. Akithibthisha kisa hicho kamanda wa polisi eneo bunge la Jomvu Lydia Wanjiru amesikitishwa na mauaji ya afisa wa...

Hatimaye muungano wa mabaharia nchini SUK waandaa uchaguzi wake

Hatimae Muungano wa mabaharia nchini SUK umeandaa uchaguzi wake rasmi katika ukumbi wa Licodep eneo bunge la Likoni kama ilivyoratibiwa baada ya uamuzi wa mahakama ya leba.Katika uchaguzi huo,...

Gavana wa Kwale Fatuma Achani amesema kuwa uzinduzi wa mradi wa kisima cha maji katika eneo la Melikubwa huko Macknon unalenga kukabiliana na baa la njaa katika eneo hilo ambalo hukumbwa na kiangazi kikali mara kwa mara.

Kulingana na Achani mradi huo utawasaidia wakaazi kupata maji ya mifugo na kuyatumia katika maswala ya kilimo badala ya kutegemea chakula cha msaada kutoka kwa serikali na wahisani.

Akizungumza katika eneo hilo, Achani amesema kuwa wakaazi watapata kuzalisha chakula cha kutosha kwa kuzingatia kilimo cha unyunyuziaji maji mashamba.

Kwa upande wao baadhi ya wakaazi eneo hilo wamedai kuhangaikia bidhaa hiyo muhimu kwa kutembea mwendo mrefu.

Hata hivyo wakaazi hao wakiongozwa na Mwajoto Mwagawari wamesema kwamba watatumia mradi huo hususan kufanya ukulima.


RadioRahma ads