Mwili wa afisa wa polisi wapatikana na majeraha kichwani Kibarani

Mwili wa afisa wa Polisi umepatikana umetupwa katika eneo la Kibarani hapa Mombasa. Akithibthisha kisa hicho kamanda wa polisi eneo bunge la Jomvu Lydia Wanjiru amesikitishwa na mauaji ya afisa wa...

Serikali ya kitaifa na kaunti zatakiwa kushirikiana kuwawezesha wavuvi kwa vifaa vya kisasa

Ipo haja ya serikali ya kitaifa na zile za kaunti kushirikiana kuhakikisha inawekeza zaidi kwa kuwawezesha wavuvi kupata vifaa kuvua katika bahari kuu.Gavana wa Lamu Issa Timamy ambaye pia ni...

Huku ulimwengu ukiadhimisha uhuru wa vyombo vya habari, shirika la waandishi wa habari la Kenya Correspondent Association limezitaka taasisi za serikali kuhakikisha kuwa uhuru wa wandishi habari umelindwa vyema.

Mwenyekiti wa shirika hilo kanda ya pwani Baya Kitsao amesema kuwa kwa miezi ya hivi karibuni waandishi habari wamekuwa wakipitia madhila mengi mikononi mwa maafisa wa polisi katika eneo la pwani.

Kulingana na Baya visa vingi vya wanahabri kudhulumiwa kikazi viliweza kushuhudiwa hasa wakati wa uchaguzi mkuu uliopita ambapo wanahabari walishambuliwa na maafisa wa polisi wakiwa kazini.

Mwenyekiti huyo pia amekashifu vikali hatua ya wizara ya usalama wa ndani ya kuwakataza wandishi habari kuangazia moja kwa moja mauaji ya halaiki katika eneo la shakahola.

Mwandishi habari Francis Mwaro amewataka wananchi kushirikiana na wandishi habari katika kuendeleza kazi zao badala ya kuwavamia kwa misukumo ya hisia tofauti tofauti.
Kulingana na Mwaro amepitia hali ngumu hasa katika kuangazia mauaji ya halaiki ya shakahola na pia kuangazia matukio katika kanisa la New life church lililoko Mavueni.

Mwandishi habari Triza Auma amewataka wamiliki wa vyombo vya habari nchini kuhakikisha kuwa wamewalipa vizuri wandishi wao.
Kulingana na Triza wanahabari wengi wanapitia masaibu mengi tokea kuanza kwa wimbi la virusi vya Corona.

 


RadioRahma ads