Mwili wa afisa wa polisi wapatikana na majeraha kichwani Kibarani

Mwili wa afisa wa Polisi umepatikana umetupwa katika eneo la Kibarani hapa Mombasa. Akithibthisha kisa hicho kamanda wa polisi eneo bunge la Jomvu Lydia Wanjiru amesikitishwa na mauaji ya afisa wa...

Serikali ya kitaifa na kaunti zatakiwa kushirikiana kuwawezesha wavuvi kwa vifaa vya kisasa

Ipo haja ya serikali ya kitaifa na zile za kaunti kushirikiana kuhakikisha inawekeza zaidi kwa kuwawezesha wavuvi kupata vifaa kuvua katika bahari kuu.Gavana wa Lamu Issa Timamy ambaye pia ni...

Waziri wa madini na masuala ya uchumi wa bahari Salim Mvurya ameutetea mswada wa fedha wa mwaka 2023 akisema kuwa unalenga kupunguza gharama ya maisha.

Mvurya amewataka wale wanaopinga mswada huo kuusoma kwa kina badala ya kulalamika.

Waziri huyo amesema kuwa tayari serikali imeondoa ushuru kwa bidhaa mbali mbali kama njia moja ya kukabiliana na hali ngumu ya kiuchumi nchini.

Aidha Mvurya amesema kuwa wananchi watapewa fursa ya kuchangia maoni ili kurekebisha mswada huo kulingana na katiba.

Haya yanajiri huku mswada huo ulioidhinishwa na baraza la mawaziri ukitarajiwa kujadiliwa na wabunge baada ya kuwasilishwa bungeni.


RadioRahma ads